30 Septemba 2025 - 16:39
Kufanyika kwa warsha maalumu yenye mada “Vigezo, Mifano na Mchakato wa Nadharia za Kimataifa” huko Qom

Kitengo cha Utafiti cha Jame’atuz-Zahra (s) kwa kushirikiana na Shirika la Utamaduni na Mawasiliano ya Kiislamu, kinatarajia kuandaa warsha maalumu ya kitaalamu na ya kiutendaji yenye mada “Vigezo, Mifano na Mchakato wa Nadharia za Kimataifa” katika muktadha wa Tuzo ya Kimataifa ya Shahidi Sadr.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Warsha maalumu na ya kiutendaji yenye mada “Vigezo, Mifano na Mchakato wa Nadharia za Kimataifa” ikiangazia Tuzo ya Kimataifa ya Shahidi Sadr, itafanyika siku ya Jumapili, tarehe 13 Mehr 1404 (saa 2:00–5:00 asubuhi) katika jengo la maktaba, Kitengo cha Utafiti cha Jame’atuz-Zahra (s).

Warsha hii itafundishwa na Hujjatul-Islam wal-Muslimin Dkt. Yahya Jahangiri kwa lengo la kuwawezesha watafiti, wanafunzi wa ngazi ya tatu, ngazi ya nne na wale wa fiqhi ya juu katika uwanja wa nadharia za kimataifa.

Muda wa mwisho wa kujisajili katika warsha hii umewekwa hadi tarehe 12 Mehr 1404, na wanaopenda kushiriki wanaweza kujisajili kupitia anuani ya mtandaoni: forms.jz.ac.ir/f_25.

Kufanyika kwa warsha maalumu yenye mada “Vigezo, Mifano na Mchakato wa Nadharia za Kimataifa” huko Qom

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha